Thursday, November 10, 2011

RIHANNA - MAN DOWN LYRICS

RIHANNA - MAN DOWN LYRICS

Monday, November 7, 2011

DJ CASHMIZO: Wema analipi lakutueleza ebu tumsikilize!!!!!!!!!!...

DJ CASHMIZO: Wema analipi lakutueleza ebu tumsikilize!!!!!!!!!!...

I would be killed very resourceful in my imagination

DJ CASHMIZO: Ray back na nyimbo yake mpya (Dj Kali Kali)

DJ CASHMIZO: Ray back na nyimbo yake mpya (Dj Kali Kali)

I would be killed very resourceful in my imagination

WALIKUA KWENYE TUMBO MOJA CHAKUSHANZA!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Mwanamke nchini India, Rinku Devi (28) amejifungua watoto wawili wa kiume waliokuwa katika miji tofauti ya mimba.
Kwa mujibu wa madaktari, mama huyo alipata ujauzito miezi tofauti, na kwamba wamepishana umri wa mwezi mmoja!
Ingawa watoto hao walizaliwa kabla ya muda wao, wanaendelea vizuri.
Rinku alijifungua watoto hao Ijumaa iliyopita kwa operesheni, na kwa mujibu wa maelezo ya madaktari, uzao kama huohutokea angalau mara moja katika kila watoto milioni 50.
Madaktari wamesema, ni nadra sana kwa mwanamke kupata mimba ya watoto 'pacha' wanaokuwa katika miji tofauti ya mimba.
Mama huyo alifahamu kuwa alikuwa na ujauzito wa watoto pacha lakini hakujua kwamba kila mmoja alikuwa kwenye mji wake!
Amesema, wakati akiwa katika maumivu ya uchungu wa kujifungua alielezwa kuwa watoto wake watarajiwa walikuwa miji tofauti, akaogopa na hakufahamu angefanya nini kwa kuwa hakuwahi kusikia kitu cha namna hiyo.
Kwa mujibu wa mama huyo, alipoambiwa kuwa alikuwa na ujauzito wa watoto wawili pacha, alidhani kuwa wanawe wangefanana, lakini 'madogo' hawafanani.
Mama huyo mwenye mtoto mwingine wa kiume mwenye umri wa miaka minne anamshukuru Mungu kwa kumpa maisha mapya.
soma hapo chini
An Indian woman with two wombs has given birth to two sons - one from each uterus.
Delighted mother Rinku Devi delivered her one-in-fifty-million babies last Friday in the northern city of Patna.
Stunned doctors said giving birth to healthy babies conceived in different ovaries is so rare an average of one case is reported each year anywhere in the world.
Rinku, 28, believed she was carrying twins but had no idea of her medical condition, known as uterus didelphys, or double uterus.
Rinku Devi gave birth to two sons in India last Friday - one from each of her uteruses
During labour doctors discovered the mother-to-be had conceived her sons a month apart, during successive menstrual cycles.
'I got to know about having two uteruses when I was already in labour pain,' she said.
'I didn't know how to react. I was in pain and quite scared. I had not heard of anything like this before.
I got to know about the rarity and severity of this condition days after my delivery.
'I am very happy and feel proud to have survived through this. When I was told I was carrying twins, I thought they would look the same, but I am happy they look different.
I want to thank God for giving me a new life,' she added. 
 The 28-year-old had no idea of her rare condition until she was actually in labour
The babies, although premature, are healthy and were born by caesarean section Uterus didelphys (sometimes also uterus didelphis) manifests as a double uterus with two separate cervixes, and in some cases a double vagina too.
Each uterus is linked to the fallopian tube that faces its ovary. The phenomena occurs when the embryogenetic fusion of the mullerian ducts fails to occur.
Patients with a double uterus may need special attention during pregnancy as premature birth is common. 
 
 Cesarean sections are performed in 82 per cent of patients. The condition is also associated with higher rate of infertility, spontaneous abortion, intrauterine growth retardation, and postpartum bleeds.
'I only found out about Rinku's condition when she was in labour, it wasn't diagnosed until then,' she said.
'I knew from her reports that she was carrying twins, but when I understood the situation I was a little taken aback. I had never handled such a case before.
'Even my mother-in-law, who retired last year as the head of gynaecology at the city hospital, never experienced such a case. It is very rare.'
Dr Singh said most women with the condition were not even aware of it as it rarely caused other symptoms.
'Rinku was not aware that she has two uteruses despite the fact that she had delivered her first baby four years ago,' said Dr Singh.
'She had a normal pregnancy before. The chances of carrying a baby in each of the wombs at the same time are one in fifty million.'
Such pregnancies are often fatal for mother and baby, carrying a high risk of miscarriage, premature labour and underweight babies.
Dr Singh said: 'Fortunately this was a different case because Rinku was healthy and her babies had grown well.
To minimise the risk or stress to mother or babies we decided to operate. The caesarian surgery lasted for about an hour and two boys weighing 1.5 and 2 kilograms were born.'
Rinku, the wife of an army intelligence officer, lives with her family in Mathurapur Chakiya village of Bihar.

WEMA NA DIAMOND NGOMA DROO


WATANO WA WEMA NI HAWA
Kwa kinywa chake, Wema anakiri kutoka kimapenzi na wanaume kadhaa huku akiomba chondechonde: “Jamani TID (staa wa Bongo Fleva, Khaleed Mohamed) na Blu (Herry Samir, naye msanii wa Bongo Fleva) naomba muwatoe kabisa kwani hawakufaidi penzi langu.”
Kwa kauli hiyo, ukiwaondoa TID na Blu ambao nao aliwahi kudaiwa kutoka nao, listi inayobaki ambayo ilithibitishwa na Wema mwenyewe ni kama ifuatavyo;
KANUMBA
Steven Charles Kanumba, akitumia cheo chake cha uigizaji na udairekta katika tasnia ya filamu za Kibongo, mwaka 2008 alifanikiwa kumshawishi mlimbwende huyo kuingia kwenye uigizaji na baadaye wakazama katika ‘malavidavi’ kabla ya kumwagana kwa skendo huku Kanumba akimburuta Wema mahakamani kwa kuvunja kioo cha gari lake.
JUMBE
Mjasiriamali Jumbe Yusuf Jumbe alifanikiwa kuonja penzi la Wema mwaka 2009 na kama ilivyokuwa kwa Kanumba, naye alimwagana na mnyange huyo kwa kashfa na maneno ya shombo kedekede.
HARTMANN
Mara baada ya kuchomoka mikononi mwa Jumbe, mwaka huo huo wa 2009, Wema alidaiwa kuangukia kwa ‘the big boss’ wa Hartmann Production, Hartmann Othmun Mbilinyi lakini baadaye alijiweka pembeni kuepuka msongamano na safari ya mapenzi ikaendelea.
CHALZ BABA
Siku chache kabla ya kutimkia nchini Marekani mwaka 2010, Wema alitangaza kuolewa na mwanamuziki wa Bendi ya African Stars International ‘Twanga Pepeta, Charles Gabriel Mbwana ‘Chalz Baba’ baada ya kukolezwa na ‘malavu’. Akaondoka nchini, aliporejea, alikuwa amekwishabadili upepo na moyo wake ulishamdondokea mtu mwingine hivyo wakatengana kwa maneno ya hapa na pale.

DIAMOND
Wakati Diamond akiwa juu kimuziki mwaka 2010, ghafla zikavuja habari kuwa yeye na Wema huwa wanachati kwa muda mrefu kwenye Mtandao wa Facebook, baadaye wakasimama mbele ya kamera ya gazeti ndugu na hili, Risasi na kuanika mapenzi yao.


WATANO WA DIAMOND NI HAWA
Kabla ya kukutana na Wema, Diamond aliwahi kuripotiwa akidaiwa kupeana ‘kampani’ na warembo wafuatao;
REHEMA
Akiwa amepata jina kupitia Miss Kiswahili 2009, Rehema Fabian ‘Video Queen’, mwaka huo alikiri kuwa: “Jamani Diamond ni mtu wangu ‘so’ wasichana wa mjini kaeni mbali naye.” Alipoulizwa Diamond anayetamba na ngoma yake mpya ya Moyo Wangu, akacheka sana, akakata simu na penzi lao lilisambaratika 2010.
WOLPER
Mwaka huo huo, wakati kukiwa na ‘rumansi’ kuwa Diamond anapeana ‘tafu’ na staa mkubwa wa filamu za Kibongo, Jacqueline Masawe Wolper, ghafla Rehema akafungua kinywa: “Wolper niachie Diamond wangu.” Baada ya kauli hiyo, Diamond na Wolper wakafyata mkia na hawakusikika tena.
PENDO
Mwaka jana, pia Diamond aliripotiwa akidaiwa ‘kutoka’ na staa wa Maisha Plus Season II, Upendo Mushi ‘Pendo’. Diamond alipotafutwa ili kupata mzani wa habari hiyo, akaruka futi mia na ukawa mwisho wa penzi lao.

NATASHA VS WEMA
Mwanzoni mwa mwaka huu, gazeti tumbo moja na hili, Amani lilitonywa kuwepo kwa mrembo aliyetajwa jina moja la Natasha ambaye alidaiwa ‘kumfia’ Diamond. Hata hivyo, wakati mawasiliano kati ya Diamond na Natasha yakiendelea, Wema ambaye ndiye alikuwa amejitwalia penzi la msanii huyo, akaenda mstari wa mbele na kuharibu kila kitu.
Wema na Diamond ni wapenzi ‘hoti’ kwa sasa ambao wameahidi kufunga ndoa ‘soon’.

Hivi ni wasanii wangapi wanaoijua thamani yao?

HAKUNA ubishi kwamba, miongoni mwa fani mbalimbali za sanaa katika jamii ya Kitanzania kwa zama hizi, ni sanaa ya maigizo, hasa filamu ndiyo inayoonekana kutesa zaidi. Pamoja na sanaa ya filamu, pia sanaa ya muziki, hasa wa kizazi kipya imeonekana kutingisha miongoni mwa vijana.

Sanaa ya filamu hapa nchini imetokea kujitwalia wapenzi kibao kiasi cha kuwa kimbilio la vijana wengi, wake kwa waume, watoto kwa wakubwa na hivyo kuonekana kuwa mkombozi wa ajira kwa vijana hao huku wengi wakiwapongeza waigizaji wake kuwa, wameweza kuipa jamii ya Kitanzania kitu kipya.

Siyo siri, kwa nchi za Ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati, uchunguzi umeonesha kuwa ni Tanzania iliyo mstari wa mbele katika nyanja ya tasnia ya filamu ambayo imeonekana kuwa na mchango mkubwa kwa jamii yetu, licha ya kuwepo mapungufu mengi kiutendaji.
Filamu (Movie au Motion pictures) ni mfululizo wa picha zinazoonesha mwendo wa watu au vitu na kuonekana mbele ya watazamaji kwenye skrini. Ni aina ya mawasiliano yanayotumiwa kutolea hadithi au kuwaelezea watu kuhusiana na kujifunza fikra au mitazamo mipya katika jamii. Watu katika kila pembe ya dunia huwa wanaangalia filamu ambazo zinaelezea hadithi fulani ikiwa kama kiburudisho, au njia mojawapo ya upenzi.

Katika duru nyingi za kimataifa, nchi yetu ilipata kusifiwa kwa jitihada zake za kushughulikia ukuzaji wa utamaduni, filamu zikiwemo. Hata hivyo, kwa hali ilivyo sasa na kama hatua za dhati hazitachukuliwa, kazi iliyofanywa miaka ya nyuma, hasa mara baada ya uhuru hadi miaka ya 90, itapotea na tutajikuta tukiwa taifa lenye raia wasio na mwelekeo, wasiojifahamu au heshima mbele ya mataifa mengine.

Hivi karibuni kuliitishwa mkutano wa wasanii na wadau wa filamu kwenye viwanja vya Leaders Club na shirikisho la filamu Tanzania, ambapo pamoja na mambo mengi yaliyokemewa ni suala la mahusiano ya kingono miongoni mwa wasanii, jambo ambalo limekuwa likifanywa waziwazi huku likipamba vichwa vya habari vya magazeti.
 
Hemedi Suleiman na Jacky Penteze
Uwepo wa tungo za kimapenzi katika kazi nyingi za sanaa (filamu na muziki) ni changamoto kubwa katika utamaduni wetu kwani imezifanya kazi za wasanii kuwa za kusisimua na kuamsha utendaji ngono miongoni mwa wanajamii na kuwaacha wao wakiwa waathirika wakubwa. Wasanii wanapaswa wajiulize, kwa nini filamu na nyimbo zetu nyingi ni za mapenzi peke yake au zisizo na asili yetu bali zilizonakili vitendo na maudhui ya jamii za nje?
Cha ajabu wasanii wamekuwa mstari wa mbele kutoa elimu dhidi ya Ukimwi kwa jamii na kujisahau wao binafsi kwamba wako katika mazingira hatari ya kupata maambukizi.
Ieleweke kuwa wasanii wa Kitanzania ni mojawapo ya kada ya wasanii ambao wanatajwa kuwa hatarini kuambukizana virusi vya Ukimwi kutokana na umaarufu walionao na kujikuta wakishawishika kuingia katika vitendo mbalimbali vya hatari kwa afya zao hasa vya ngono.
Imekuwa ikielezwa kuwa umaarufu, ushawishi na kutojitambua miongoni mwao kimekuwa chanzo kikubwa cha wao kuwa hatarini kupata maambukizi hayo. Kutojitambua huwafanya wawe hatarini kuathiriwa na ugonjwa wa Ukimwi kwani hufuatwa na kundi la watu na mara nyingi kujikuta wakishawishiwa kufanya ngono katika mazingira yasiyo salama.

Kada ya wasanii imekuwa ikiathiriwa sana na ugonjwa huu toka umegunduliwa kwani katika nchi zilizoendelea kumekuwa na taarifa za vifo vya wasanii wengi vinavyotokana na Ukimwi, ambapo kutumia vibaya umaarufu kumekuwa kukichanganywa na matumizi ya vilevi.
Yote haya ni sababu ya kupotea kwa utamaduni wetu kwani utamaduni ndiyo “kidhibiti mwendo” kinachoongoza mwenendo na tabia za watu katika jamii. Ndiyo msingi wa maisha ya mtu binafsi. Humuwezesha kujitambua, kuwa na mwelekeo na kujichagulia falsafa sahihi ya maisha yake. Ndiyo msingi wa maendeleo na ubunifu katika jamii. Maendeleo ya uchumi katika maana yake pana ni matokeo na sehemu ya utamaduni wa watu. Maendeleo yasiyojengwa katika misingi ya utamaduni wa jamii ni maendeleo yasiyokuwa na maana kwa jamii hiyo.

Swali la kujiuliza, je, sanaa zetu zilivyo leo zinaweka kumbukumbu nzuri itakayorithiwa na vizazi vijavyo na kuashiria Historia inayolingana na mila na desturi nzuri za kizazi husika? Au kizazi hiki kinaweka kumbukumbu potofu ya sanaa zetu na uasili wake kwa vizazi vijavyo?

Sanaa kama nguzo mojawapo muhimu ya Utamaduni hukua na pia huweza kufa. Je, kutokana na hoja hii sanaa zetu zinakua au zinakufa au zipo katika chumba cha wagonjwa mahututi? Nadhani kwa hali halisi ilivyo kila mtu atakuwa anayajua majibu sahihi ya maswali haya.

Kuwepo madai au tuhuma za mara kwa mara kwamba, baadhi ya watayarishaji na waongozaji wa filamu wana tabia ya kuomba penzi kutoka kwa wasanii wa kike, ndiyo wawape nafasi ya kushiriki katika filamu zaao au msanii huyo anaweza kuanza kushiriki filamu halafu baada ya muda unasikia yeye na mtayarishaji au muongozaji wake wana mahusiano! Habari hizi zimekuwa zikiripotiwa sana kwenye vyombo vyetu vya habari, hasa magazeti.

Kuna ulazima gani kwa msanii eti kwa sababu kapewa kushiriki filamu halafu baada ya muda anakuwa na mahusiano na mtayarisahji, nini kinasakwa hapa? Ni kweli watayarishaji wanawalazimisha wasanii wa kike au wasanii wenyewe wanajilegeza kwao? Na kama hawakubaliani na mambo hayo kwa nini hawakatai? Kama hawakubaliani na hali hii si wanajua majibu yake?
Miaka ya nyuma waliokuwa wakiingia kwenye sanaa wengi wao walisukumwa na vipaji walivyonavyo na waliipenda sanaa bila kujali kama watapata umaarufu au la, na waliongozwa na maadili ya utamaduni wao tofauti na siku hizi, ambapo wengi wanaokimbilia kuigiza (hasa wasanii wa kike) wanasukumwa na lengo la kutaka umaarufu ili wapate 'mapedeshee'. Kwa maana nyingine sanaa ya filamu ni sawa soko la kutafuta mabwana.

Msanii makini huwa anajiwekea malengo makubwa katika maisha yake, ambapo atakuwa makini zaidi na daima atajiepusha na tabia zinazoweza kumpelekea kutofikia malengo yake. Hali hii haina maana kwamba hatajihusisha na starehe zinazoambatana na ujana! La hasha. Ila hata kama anakwenda 'club' au kwenye starehe yoyote basi atatambua lengo lake na atajua dosari inayoweza kumpata endapo atajilegeza na kufuata vishawishi.
Diamond na Wema Sepetu
Mi' nadhani jamii yetu imepotoka na inahitaji msukumo mpya kuirudisha katika maadili ya kweli. Maadili yamepotoshwa tangu kwenye ngazi ya familia tunazotoka, hali hii humfanya kijana kujiona hafai kwa chochote katika familia anamotoka au katika jamii ya watu inayomzunguka.

Hisia hii inampelekea kujichukia na kupata msukumo wa kutaka kutafuta thamani ya nafsi yake kirahisi. Njia mojawapo ya kufanya hivi ni kujaribu mambo ya mapenzi. Kwa msichana wa hali hii ni rahisi kufikiri thamani yake inatokana na tendo hili la ngono kwani linaambatana na lugha nzuri wanazotumia wavulana na ahadi au zawadi anazoweza kupewa.

Ni wakati sasa wa Serikali kuangalia namna ya kuwasaidia wasanii ambao ndiyo kioo cha jamii, hasa jamii ya vijana kwa kuandaa semina zinazohusu kujitambua na kuwasaidia kuanza safari ya kutafakari, “Mimi ni nani?,” na “Thamani yangu inatokana na nini?” Hii itawasaidia kutambua kwamba thamani ya mtu haitegemei watu wengine wala wanavyosema, hata si umbo alilo nalo, bali ni hali ya ndani. Thamani ya mtu ipo ndani ya utu wake, yaani nafsini mwa mtu mwenyewe.
 

WABONGO VIPI TENA USIPATE JINA TU!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Prodyuza ambaye pia ni msanii anayefanya vizuri kunako gemu la muziki wa Bongo Fleva, Raheem Nanji ‘Bob Junior’ (pichani) amefunguka kuwa, yeye si shoga ila kazi yake ndiyo inamfanya awe kama alivyo.

Akizungumza na na Ijumaa juzikati maeneo ya Magomeni jijini Dar es Salaam, Bob Junior alisema kuwa, baadhi ya watu wamekuwa wakimtafsiri tofauti kutokana na muonekano wake bila kujua kuwa, usanii ndiyo chanzo.

Alisema kuwa, yeye ni mwanaume kamili na watu wasiende mbali katika kujadili muonekano wake na kumuingiza kwenye ushoga bali watathmini burudani anayotoa.

“Watu wanashindwa kuelewa kama usanii ni kazi kama zilivyo kazi nyingine, lazima mtu uwe tofauti kuanzia muonekano, mavazi na hata staili yako ya kutoa burudani kwa mashabiki, kama ni shoga mbona hata leo tu nilikuwa na baby wangu?” alisema Bob Junior.

Hivi karibuni gazeti dada na hili (Risasi Jumamosi) liliripoti kuwa, Bob Junior alibambwa maeneo ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam nyumbani kwa Miss Kiswahili 2009, Rehema Fabian lakini wawili hao walipohojiwa hawakuweka wazi uhusiano wao licha ya huko nyuma kudaiwa kutoka kimapenzi.

Regina Mwalekwa atimba Clouds FM

Ni kawaida kwenye free market watu ku move. Lakini wakati mwingine binadamu na ajira anafananishwa na ngombe wa kufugwa mmoja anapoona mwenzake kapewa majani anakula anafikiria yale ya mwenzake ni matamu zaidi na akipata mwanya huenda mbio kuonja. Njia pekee inayoweza mwajiri kujali wafanyakazi ni wakianza kuhama. Kama Mengi alikuwa anawabania huenda akabadilika

New song kutoka next week, by Endru G

Nisikitika kuwa taarifu kuwa utambulisho wa video yake mpya utakuwa next week,kutokana msichana aliyecheza kwenye video yake,amefiwa na mama yake mzazi na walisha safirisha msiba kwenda Songea pole sana Shora n R.i.p Vick Nyoni aka Mshua,tulikupenda lakini mungu kakupenda zaidi

Bathday Party

Tukumbuke kulala mchana kama unajuwa baadae utatoka kwenda kwenye party jama 
Big Alexander Nice God boy
 
Nice Gog Party


I would be killed very resourceful in my imagination

New Video Blad Key - Vinapanda bei